Stori: Gladness Mallya
NDOA ya msanii mkongwe wa filamu Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ ipo katika mtikisiko mkubwa kufuatia
mawifi zake kumpenda zaidi mwanamke aliyezaa na mumewe kabla hajaolewa.
Msanii mkongwe wa filamu Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’.
Chanzo makini kinasema Cathy yupo katika wakati mgumu kwani amesimama
na mumewe tu na hakuna hata wifi mmoja ambaye anamkubali, bali wote
wameelekeza nguvu kwa mwanamke huyo na mara nyingine huwa wanamchukua
kumpeleka nyumbani kwao Morogoro.
‘Cathy’ akipozi.
Cathy alipopatikana alikiri na kusema hata hivyo hao mawifi
wanajisumbua bure kwani hawezi kuachika kwa ajili yao, kwa sababu mumewe
Rupia anampenda sana labda siku apende yeye mwenyewe na hata akiamua
kuachika mumewe hawezi kurudia matapishi, atachukua kitu cha ukweli.Posted byMr.Prime on August 20, 2014


0 comments
Post a Comment